0


Wakala wa huduma za bara bara mkoani Manyara [TANROADS[ wamekabidhi kisima cha maji katika kijiji cha Boay wilayani Babati mkoani Manyara chenye gharama ya shilingi milioni 42.631.
Mradi huo wa kisima cha maji katika kijiji cha Boay ni makubaliano kati ya Tanroads mkoa wa Manyara na kampuni  ya ujenzi wa bara bara china road seventh  group L.t.d kutoka nchini China ambayo inajenga bara bara ya lami kutoka Bonga mkoani Manyara hadi Dodoma.

Akizungumza wakati anakabidhi kisima hicho kwa mhandisi wa maji halmashauri ya wilaya ya Babati Samwel Tluway,meneja wa Tanroads mkoani Manyara Bashiru Rwesingisa ameitaka Halmashauri kukitunza kisima hicho na kukikagua kila mwaka na kuhakiki ubora wa maji.
‘Uchimbaji wa kisima ni moja kati ya majukumu ya mkandarasi anaejenga bara bara kutoka Mela Bonga-Dodoma,na kimsingi visima hivyo ni kwa ajili ya kusaidia shughuli za ujenzi wa bara bara”alisema Rwengisira.

Kisima hiki kilipatikana baada ya uchunguzi uliofanyika na watafiti wa kijiolojia kutoka chuo cha Maji Ubungo  mwezi oktoba 15, 2015 ambao waliobaini kuwa maji hayo ni safi na salama kwa matumizi ya bindamu.
Mashine ililiyofungwa kupandisha maji kutoka ardhini katika Kisima hicho inatumia nishati ya jua nishati jadidifu ili kuepuka gharama za umeme wa Tanesco.
Mkandarasi huyo amechimba visima sita  katika vijiji vya Manyara na Dodoma,vijiji hivyo ni  Ukunku,Kolo,Masawi visima viwili,Boay pamoja na Bereko.
Kisima hicho walichokabidhiwa wanakijiji wa kijiji cha Boay  kina sifa za kipekee, kina uwezo wa kutoa maji hadi lita 6,000 kwa saa,lina uwezo wa kuhifadhi maji lita elfu hamsini 50,000,pamoja na pampu yenye uwzo wa kupampu maji lita 2,100 kwa saa.

Mwenyekiti wa kijiji cha Boay Emmanuel Nikodemus Kaji ameishukuru kampuni hiyo ya China road seventh group Ltd  pamoja na serikali kupitia Tanroads kwa kuwapelekea huduma muhimu ya maji wakazi wa kijiji hicho.
‘Naishuru sana serikali kwa kutukumbuka wananchi wa vijijini katika huduma muhimu za kijamii kama hizi”.
Akizungumza kwa niaba ya Nao wakina mama mjumbe wa serkali ya kijiji cha Boay Bi Zamda Fante amesema kisima hicho kitawasaidia kuwapunguzia usumbufu waliokuwa wanaupata kutafuta maji umbali mrefu.
Alisema kwa kapatiwa kisima hicho cha maji watapata nafasi ya kufanya zaidi kilimo cha umwagiliaji.

Pia amewataka wanakijiji wenzake waulinde mradi huo waliopewa kama zawadi na kampuni hiyo ya ujenzi wa bara bara kutoka nchini china.
Akizungumza kwa niaba ya Mkurugezi wa Halmashauri ya wilaya ya Babati mhandisi wa maji Samwel Tluway amewahidi wakandandarasi pamoja na Tanroads kuwa mradio huo wataulinda,kuendeleza na kuuboresha zaidi.
Meneja mradi wa kampuni ya China Road Seventh  Group[CRSG] Bwana Dong Hui ameishukuru Tanroad Mkoa wa Manyara kwa kuwapa ushirikiano katika kipindi chote walichokuwa wakitengeneza bara bara hiyo kutoka Mela bonga mpaka Dodoma ambapo kwa sasa imekamilika na inatarajiwa kuzinduliwa na rais wa Tanzania John Magufuli kati ya mwezi oktoba na Novemba mwaka huu.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top