0
GHAROS RIWA & THOMAS MASALU-
BUNDA
Jumla ya wazee 235 katika kata ya neruma wilayani Bunda Mkoani Mara  wamepatiwa vitambulisho vya msamaha wa matibabu lengo ikiwa ni kuhakikisha wazee wanatambuliwa na kupewa fursa ya kushiriki katika mambo yanayohusu maisha yao ya kila siku.
Akisoma taarifa ya utoaji wa huduma za afya na stawi wa jamii Kwa mgeni Rasmi Kaimu Afisa Ustawi wa Jamii wilaya ya bunda Liberatus Kazana katika maadhimisho ya siku ya wazee Duniani yaliyofanyika Katika kijiji cha Neruma kata ya neruma Oktoba 20 amesema Halmashauri ya wilaya ya Bunda inajumla ya wazee 9,994 waliona miaka 60 na kuendelea.
Kazana Amesema kunachangamoto mbalimbali katika uendeshaji wa huduma za afya na hasa katika kuwahudumia wazee huku gharama za uendeshaji wa huduma za msamaha zimekuwa kubwa katika vituo vya kutolea huduma za afya hiyo ikitokana na idadi kubwa ya wagonjwa wanaohitaji msamaha kama vile akina mama wajawazito,watoto chini ya miaka mitano,walemavu na wazee.

Kwa upande wake  mgeni rasmi katika maadhimisho hayo ambaye ni Katibu Tawala wa wilaya ya Bunda Masalu Kisasira amesema wao kama serikali wanatambua changamoto hizo hivyo ameahidi kuzifanyia kazi huku akiwasihi wazee kuwa kioo kizuri kwa watoto wao kwa kuwaonya na kuwashauri ili kuwawezesha watoto wao kuwa na misingi bora ya maisha.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top