0
Unaweza kusema ni rekodi ya burudani wameiweka katika mji wa Babati mkoani Manyara Roma na Stamina [ROSTAM] walipofanya bonge la Show katika ukumbi wa River nile Hall na kuwajaza mamia ya mashabiki wa Babati na viunga vyake.

ROSTAM wanaotamba na wimbo wao wa Kibamia waliomshirisha Maua Sama walitikisa zaidi pale amabpo walikamata maiki na kuimba kwa kupokezana kama ilivyokuwa kawaida yao.

Naye Shilole hakubaki nyuma alihakikisha  anakonga nyoyo za mashabiki wake kwa kutawala jukwaa zima akiwa na dancers wake wawili.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top