0

Mbunge wa Nzega (CCM), Hussein Bashe
amewahakikishia wananchi wa Tanzania kuwa hoja yake aliyoiwakilisha kwa Katibu
wa Bunge kuwa haiwezi kukwamishwa na jambo lolote kwa madai hakuna
kisichojulikana kinachoendelea kutoka katika nchi.

Bashe ametoa kauli hiyo leo (Machi
08, 2018) wakati alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es
Salaam kwa lengo la kuelezea sababu zilizompelekea yeye kama Mbunge kuandika
barua ya kutaka kuundwe kwa kamati ya uchunguzi dhidi ya matukio mbalimbali
yanayoonesha kutishia umoja, usalama na mshikamano wa taifa la Tanzania.


Kwa upande mwingine, Bashe amesema
anasubiria majibu ya barua aliyotuma kutoka kwa Katibu wa Bunge Pamoja na
Katibu Chama cha Mapinduzi (CCM) ambayo ameeleza dhamira na nia yake huku
akisisitiza zaidi kuwa jambo hilo hajalifanya kwa mihemuko (kukurupuka) bali
amefanya kwa umakini wa hali ya juu na utafiti wa kutosha.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top