Waziri mwigulu Nchemba alisema hayo wakati akifanyiwa mahojiano na kudai kuwa miili ya watu ambayo imekuwa ikiokotwa baharini si miili ya Watanzania kwani kama ingekuwa miili ya Watanzania hivyo basi familia zao zingekuwa zinasikika kizipiga kelele kuhusu ndugu zao hao kupotea.
Aidha Waziri Mwigulu Nchemba ametaka ajenda za watu zisigeuke kuwa siasa na kusema kuwa ajenda za siasa zifanywe kwenye siasa na si maisha ya watu pia Mwigulu Nchemba amedai kuwa katika matukio rasmi ambayo wao waliyapata ni kuhusu kutekwa kwa watoto Arusha.
Post a Comment
karibu kwa maoni