0
Image may contain: sky and outdoorMvua kubwa ilionyesha Juzi imesababisha maafa makubwa katika kijiji cha Gendi Babati ambapo imekufa mifugo 18 wakiwemo kuku 15, mbuzi wawili na kondoo mmoja. 
Hata hivyo lawama wametupiwa Tanroad mkoa wa Manyara Kwa kushindwa kuelekeza maji katika mkondo na kuyaachia yapite katika barabara. Image may contain: one or more people, people standing and outdoor
Waliokutwa na maafa hayo wameiomba serikali kupitia mfuko wake wa Maafa iwasaidie kwani mvua hizo zimewasababishia hasara kubwa. 
Wahanga hao wameieleza Manyara Fm kuwa hawajawahi kuona hali hiyo tangu waanze kuishi eneo hilo la Gendi barazani mwaka 1993.
Nyumba zimebomoka na zingine kuweka nyufa.
Image may contain: plant and outdoor
Image may contain: 1 person, sitting, living room and indoor
Diwani viti maalum Ccm Rose Murian akizungumza na Manyara fm alipotembelewa nyumbani kwake mara baada ya kukutwa na majanga haya.
Hata hivyo kuna taarifa kuwa wakazi wa Gendi barazani wanatakiwa kuhama. 
Wamehoji waende wapi????
Image may contain: indoor
Huu ulikuwa ni mgahawa lakini kwa sasa hautoi tena huduma kwani vyombo vyote vimebebwa na Mafuriko.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top