0

Zaidi ya watu 40 wameuawa wakati wa jaribio la kuwaokoa watu waliotekwa na kundi la wanamgambo wa Boko Haram .
Takriban watu watano wa kampuni ya kuchimba mafuta waliuawa, kwa mujibu wa chuo cha Maiduguri.
Wanajeshi pia waliuawa wakati wa uvamizi huo.
Idadi hiyo kubwa ya vifo ni pigo kwa serikali ambayo inasisitiza kuwa kundi la Boko Haram limeshindwa.
Takriban watu 20,000 wameuawa na maelfu ya wengine kutekwa tangu Boko Haram ianzishe harakati zake mwaka 2009.
Katika kisa kibaya zaidi Boko Haram waliteka wasichana 276 kutoka shule ya wasichana kaskazini mashariki mwa Nigeria ya Chibok mwaka 2014.
Tangu wakati huo wamewaachili zaidi ya wasichana 100 kubadilishana na wapiganaji.
Taarifa za kina kuhusu kile kilichotokea siku ya Jumanne hazijulikani, huku ripoti za awali kutoka kwa jeshi, zikisema kuwa watu ambao walitekwa waliokuwa ni wakifanya kazia katika chuo cha Maiduguri waliachiliwa,.
Siku ya Jumanne jeshi lilisema kuwa miili ya wanajeshi 9 na raia mmoja ilikuwa imepatikana.
Lakini sasa chuo kikuu kimesema kuwa takriban wafanyakazi watano wakiwemo wasomi wawili na dereva waliuawa wakati msafara wao uliokuwa chini ya ulinzi mkali, ulikuwa ukirejea mjini Maiduguri kaskazini mashariki mwa Nigeria
Wengine kadha hawajulikani waliko.
………………………………..
Bunge la Senate nchini Marekani limepiga kura ya kuziwekea vikwazo vipya Urusi, Iran na Korea Kaskazini licha ya pingamizi kutoka Ikulu ya White House.
Bunge la waakilishi liliidhinisha mswaada huo mapema wiki hii kwa kura nyingi.
Baada ya mswaada huo kupita katika mabunge yote sasa utapelekwa kwa Rais Donald Trump kuwekwa sahihi.
Lakini bwana Trump anataka kuboresha uhusiano na Urusi na anaweza kuukataa licha na uungwaji mkono uliopata.
Vikwazo hivyo ni vya kuiadhibu Urusi zaidi kufuatia hatua za kulimega eneo la Crimea kutoka Ukrain mwaka 2014.
Lakini mjadala kuhusu vikwazo hivyo vipya unafanyika huku uchunguzi kuhusu hatua za Urusi kuingilia kati uchaguzi wa Marekani wa mwaka 2016 ukiendelea.
Bwana Trump mara nyingi amekana kuwa Urusi iliingilia uchaguzi huo kusaidia kampeni yake.
Waandishi wa masuala ya siasa wanasema kuwa ikiwa Trump atajaribu kuukataa mswaada huo basi itakuwa ishara tosha kuwa anaiunga mkono sana Urusi.
……………………….
Umoja wa mataifa umesema kuwa baada ya nchi za Urusi, Iran na Uturuki kusaidia kupunguza kasi ya mapigano nchini Syria, mamia kwa maelfu ya wananchi wake bado wanahitaji msaada wa haraka.
Mpango wa kuanzisha ukanda maalum ambao utakua unahusika na utoaji misaada hauna maendeleo mazuri.
Mkuu wa shirika la kutoa misaada amesema kuwa kwa mwezi huu hakuna msaada uliotolewa kwa sehemu 11 zilizoathirika na vita.
Ameituhumu serikali ya Syria kwa kuzuia misaada ya kibinaadam, huku pia akitaja makundi ya upinzani kwa serikali kama sababu ya kuwarudisha nyuma.






WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dokta Philip Mpango, amefanya ziara ya kushitukiza katika mitaa ya mji wa Dodoma na kubaini baadhi ya wafanyabiashara hawatumii ipasavyo mashine za kieletroniki za kukusanyia kodi ya Serikali-EFDs na kuwaonya wafanyabiashara kote nchini kuacha mchezo huo.

Dkt. Mpango aliyeambatana na baadhi ya maofisa wa Mamlaka ya Mapato hapa nchini-TRA mkoa wa Dodoma amebaini baadhi ya wafanyabiashara hao wasio waaminifu hawatoi risiti huku wengine wakiandika kiwango kidogo cha fedha kwenye risiti hizo.

Mmoja wa wafanyabiashara aliyekumbana na mkono wa Waziri Dokta Mpango, ni Bwana ISDORI SHIRIMA ambaye amekiri kufanya makosa ya kutotumia mashine hizi ipasavyo

“naomba unisamehe Mheshimiwa, sitarudia tena unajua sisi vijana tunabangaiza, lakini nimebaini nimefanya makosa” aliomba msamaha Bw. Shirima

Hata hivyo Dkt. Mpango ameiagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA mkoa wa Dodoma, kufanya ukaguzi wa kina wa mahesabu ya mfanyabiashara huyo ili kubaini kiwango cha kodi alichokwepa na kumchukulia hatua stahiki.

Aidha, Dokta Mpango ameiagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA mkoa wa Dodoma kuwapeleka ofisini kwake mawakala wote mkoani humo wanaosambaza mashine za kieletroniki za kukusanyia mapato EFDs baada ya kubaini kuwa zaidi ya mashine 100 zimeharibika na hazitumiki tangu jana.

“Kuna kitu sikielewi na hakiingii akilini, inakuwaje mashine ziharibike kwa kiwango hicho, mashine 100 kuharibika kwa siku mbili ni nyingi na ina maana nimekosa mapato mengi” alielezea kwa masikitiko Dkt. Mpango.

Aliagiza mawakala wote wanaosambaza ama kuuza mashine hizo wakutane naye ofisini kwake mjini humo ili kubaini tatizo na kuongeza kuwa haiwezekani wafanyabishara walipie mashine hizo zaidi ya mwezi uliopita lakini hawapelekewi hali inayozidi kuikosesha Serikali mapato yake.

Baadhi ya wananchi na wafanyabiashara wamepongeza uamuzi wa Serikali wa kulivalia njuga suala la kodi na kwamba wako tayari kuiunga mkono Serikali kwa kutoa risiti wanapouza bidhaa na kudai risiti zenye viwango sahihi vya manunuzi waliyoyafanya ili kuijengea Serikali uwezo wa kuihudumia jamii.

Dokta Mpango ametembelea pia baadhi ya vituo vya mafuta mjini humo na kuwakumbusha wamiliki wote wa vituo vya mafuta kuzingatia agizo la Serikali linalowataka wafunge mashine maalumu za kielektroniki zinazofungwa kwenye pampu za mafuta ndani ya siku 14 ambazo ziko ukingoni.


Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top