0
Mkuu wa Wilaya ya Njombe Bi. Ruth Msafiri amesema ataanzisha zoezi la kupita shule kwa shule na kupiga kura ili kubaini walimu wanaotembea na wanafunzi na kuwaharibia maisha yao ili wachukuliwe hatua stahiki.
 
Bi Msafiri ametoa salamu kwa baadhi ya shule ambazo waalimu wameacha kufundisha watoto na badala yake wamewageuza ndiyo wake zao huku akisema kuwa atawaagiza Wakurugenzi wake kupita katika shule mbalimbali kupigisha kura ili kuwabaini waalimu wanaofanya uharibifu huo kwa wanafunzi kisha baadae kuwatelekeza.
Kwa upande wa Afisa elimu Mkoa wa Njombe, Halfani Masuila, amekemea vitendo vya mahusiano baina ya wanafunzi na walimu na kusema kuwa serikali itamchukulia hatua kali mwalimu wa kike au wakiume atakayebainika kuwa na uhusiano na mwanafunzi.
Bw. Masuila amesema amebaini hilo katika shule nyingi zenye kidato cha tano na cha sita kuwa walimu wa kike wanajihusisha kimapenzi na wanafunzi hao wa kiume jambo ambalo pia kisheria haliruhisiwi na ikibainika hatua za kisheria lazima zifuatwe.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top