Chama cha mapinduzi CCM kupitia umoja wa wanawake Tanzania UWT kimefafanya uchaguzi wake wa wenyeviti na wawakilishi wengine ngazi za wilaya nchi nzima.
Uchaguzi huo ndani ya mkoa wa Manyara umefanyika katika
wilaya sita huku wilaya ya Simanjiro ukisogezwa
mbele hadi September 23 kwa sababu ya mabadiliko yaliyofanywa na Katibu wa
Halmashauri Kuu Itikadi na Uenezi wa chama hicho Taifa Humphrey Pole pole.
Nafasi zilizokuwa zikigombewa ni Mwenyekiti UWT wilaya ya
Babati mjini na vijijini,wajumbe katika mikutano ya ccm katika ngazi za wilaya
na taifa.
kura zilizopigwa kumchagua mwenyekiti wa Umoja wa wanawake
Tanzania [UWT] wilaya ya Babati ni 298 kura moja [ 1]iliharibika, hivyo kura
halali zilikuwa 297,mgombea Selina Bayo
akipata kura 137 huku Naomi Richard aliepata kura 158 akitangazwa kuwa mshindi na kukabidhiwa
kiti cha mwenyekiti uwt wilaya ya BABATI.
Nafasi ya mjumbe mwakilishi uwt wagombea walikuwa wawili,Fatuma hamad alishinda nafasi hiyo kwa kupata kura 150 huku
akimshinda Chiku Juma aliepata kura
146.,Uwakilishi jumuiya ya vijana CCM Uvccm amepita bila kipingamizi Penina
Masanja,Mjumbe mkutano mkuu taifa amechaguliwa Mariamu Kwimba aliepata kura 137
akiwashinda wenzake wawili.
Nafasi nyingine ni mjumbe mkutano mkuu ccm wilaya imeenda
kwa Elizabeth Manda kwa kura 141,mjumbe
wa hamlashauri kuu ya CCm ni Lucy Manda kura 204,wajumbe wa baraza walikuwa 11
na walihitajika wajumbe sita ambao ni Naomi Richard kura 154,Elizabeth Manda
kura 170,Hadija Juma kura 185,Asha
Hassan 218,Lucy Manda kura 220, pamoja
na Anna William aliepata kura 228.
Waliochaguliwa kushika nafasi hizo wameahidi kuwatetea wakina mama na kurudisha hadhi ya
Chama hicho katika maeneo yao.
Kwa mujibu wa katiba Ya Chama cha Mapinduzi uchaguzi wa
jumuiya za chama ngazi ya wilaya
unasimamiwa katibu tawala wilaya
ambapo kwa Babati uchaguzi ulisimamiwa na Cade Mshamu ambaye alitangaza matokeo na kwapongeza wagombea
walioshindwa kukubali matokeo hayo huku akikisisitiza kufanya kazi kwa bidii.
Kwa upande wa babati mji aliechaguliwa kushika nafasi ya mwenyekiti ni Claudia Haule aliepata kura 89,Mjumbe
mkutano mkuu taifa ameshinda Zainabu Zuberi kwa kura 72 huku nafasi ya Baraza
wilaya ikienda kwa Neema Ramadhani aliepata kura 97.
Naye Katibu wa UWT mkoa wa Manyara Hainess Munisi akawasihi
wanawake wa Ccm babati kuhakikisha hawarudii kufanya makosa kama mwaka 2015
ambapo kata nyingi zilichukuliwa na wapinzani.
Wengine ilikuwa ni mara yao ya kwanza kushiriki katika
uchaguzi huo na wakapita kwa kishindo.
Post a Comment
karibu kwa maoni