0
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kinaweza kukimbiwa na viongozi wake wengine watatu, wakiwamo wabunge wawili wa majimbo.
Taarifa kutoka ndani ya chama hicho na Ikulu jijini Dar es Salaam zinasema, mkakati mkali unasukwa wa kuwashawishi viongozi hao kukihama chama hicho na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Hata hivyo, mmoja wa viongozi anayeshawishiwa kuondoka amenukuliwa akisema, hajafikiria kufanya hivyo na kwamba hata ikimbidi kuondoka ndani ya Chadema, hatajiunga na CCM, bali atafanya shughuli zake binafsi.
Kupatikana kwa taarifa hizi kumekuja muda mchache baaada ya mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Pastrobas Katambi kujiunga na CCM leo Ikulu jijini Dar es Salaam.
Aidha, kupatikana kwa taarifa hizi kumekuja wiki tatu baada ya gazeti hili kuripoti kuwapo kwa mpango wa wabunge wa viongozi wa Chadema kukima chama hicho.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top