0
Image result for mashamba ya mbaaziWakulima wa mbaazi mjini Babati mkoani Manyara wameiomba serikali kuwahakikishia soko la zao hilo kwa msimu wa mwaka 2018 ili waamue kulima zao hilo ama kuacha baada ya soko la mbaazi kuporomoka mwaka huu wa 2017 na hali ya maisha yao kuwa magumu
Sambamba na hilo wakulima hao wameiomba serikali  kuwatafutia ufumbuzi wa changamoto ya upatikanaji wa soko la uhakika
Wakizungumza kwa masikitiko kuhusiana na hali hiyo wafanyabiashara Rukia Chikawa na  Josephat  Dickson wameeleza zao la mbaazi ndio zao ambalo walikuwa wakilitegemea kwa ajili ya biashara na kuweza kuwapatia mbegu za mazao mengine pamoja na pembejo  nyingine za kilimo
Aidha kwa upande wa serikali ya awamu ya tani imekuwa ikisisitiza kuwa  inamjali mnyonge na kuhakikisha haki ya mnyonge inapatikana katika kutatua changamoto mbalimbali, hivyo mkulima wa chini anaitegemea serikali katika kumtafutia  urahisi wa kuapata masoko.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top