KOCHA aliyeiwezesha Tanzania kufuzu fainali pekee za
Kombe la soka la Mataifa ya Afrika (AFCON), Joel Nkaya Bendera amefariki dunia
jioni ya leo katika hospitali ya taifa ya Muhimbili Jijini Dar es Salaam
alipokuwa amelazwa kwa matibabu.
Bendera amefariki ikiwa ni mwezi mmoja tu tangu kustaafu
utumishi wa serikali akiwa mkuu wa mkoa wa Manyara ambapo alimpisha Alexender
Mnyeti
Msemaji wa hospital ya Muhimbili, Aminieli Eligaisha amethibitisha kufariki kwa Bendera aliyewahi pia kuwa Naibu Waziri wa Michezo wakati wa Serikali ya awamu ya nne, chini ya Rais Jakaya Mrisho Kikwete.
Mungu aipumzishe roho ya marehemu mahali pema peponi Amin.
Msemaji wa hospital ya Muhimbili, Aminieli Eligaisha amethibitisha kufariki kwa Bendera aliyewahi pia kuwa Naibu Waziri wa Michezo wakati wa Serikali ya awamu ya nne, chini ya Rais Jakaya Mrisho Kikwete.
Mungu aipumzishe roho ya marehemu mahali pema peponi Amin.
Post a Comment
karibu kwa maoni