0
Tukio ambalo limewastua wakazi wa mji wa Babati mkoani Manyara jana baada ya milio ya risasi kusikika na kuzua hofu kubwa kwa baadhi yao ni la kutengeneza.
Akizungumza na WALTER HABARI Makao makuu ya jeshi l polisi mkoa wa Manyara Kamanda Agustino Senga ameeleza kuwa hayo ni mazoezi ya askari polisi kwa ajili ya utayari wa kupambana na uhalifu wa namana hiyo pindi unapotokea.
Ameeleza kuwa  wameamua kufanya hivyo maeneo ya Makazi ya watu ili watu wajifunze nao waweze kuchukua tahadhari pindi wanapoona matukio kama hayo na kuwataka kuwa mbali pindi wanapoona hali hiyo.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top