0


Image result for magufuli salamu za poleRais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ametuma salamu za rambirambi kwa Jaji Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahimu Juma kufuatia kifo cha Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani, Mh. Robert Kisanga kilichotokea tarehe 23, Januari mwaka huu, Katika Hospitali ya Regence ya Jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.
Taarifa za kifo cha Jaji Kisanga zimethibitishwa na Msajili wa Mahakama ya Rufaa John Kahyoza.
 Mbali na Mahakama ya Rufaa, Marehemu Jaji Robert Kisanga alifanya kazi Baraza la Habari Tanzania (MCT).
Jaji Robert Kisanga aliteuliwa kuwa Mwenyekiti wa kwanza wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kabla ya kustaafu mwaka 2008.

Marehemu Jaji Mstaafu Robert Kisanga akihutubia moja ya mkutano enzi za uhai wake.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top