0


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhuIgOXjLJ0giDt6KU4kshZoX4ItbwAhn9NBe9UMtrz3qP-0CixMUshpc6j44bbwUuE_ehQNTmKePRF7GtDnxbKkRboGNQS_GHhyphenhyphenBE6P4Diotx7EFvqLJnAfMYRDoQxfUkXJmqgOa-W9L3f/s640/MAJENEZA.jpgKijana mmoja aliyetambulika kwa jina moja la Boniface mkazi wa Mwananyamala kwa Msisiri anashikiliwa na jeshi la Polisi Mkoa wa Kinondoni kwa kuiba masanduku ya kuzikia (majeneza) mawili na kuyaficha nyuma ya choo cha mkazi mwengine wa mtaa huo

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamanda wa Polisi mkoa wa Kinondoni Jumanne Muliro, amesema tukio hilo limetokea kati ya ofisi mbili za kuuza masanduku hayo ambapo moja ndiyo iliyoibiwa majeneza hayo, ambayo moja ni la mtu mzima na moja likiwa la mtoto mdogo

Mmiliki wa masanduku hayo Bi. Judith Carlos amesema masanduku hayo aligundua yapo kwa jirani yake baada ya kumuahidi mtu atampa elfu 50 iwapo atamsaidia kujua nani kayachukua, na ndipo baadaye akaambiwa mahali yalipo.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top