0
mediaGolikipa wa zamani wa Simba, Yanga afariki nchini Burundi Kipa wa zamani wa Timu za Simba na Yanga na timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars, Ismail Suma amefariki leo akiwa nchini Burundi.
Mbali na kuzichezea Simba na Yanga, kipa huyo pia aliwahi kuichezea Mbagala Markets ambayo baadaye ilibadilishwa na kuitwa African Lyon ambayo aliipandisha daraja mwaka 2009.
Mchezaji wa zamani wa aliyecheza na Suma, Patrick Mrope ameiambia RFI Kiswahili kwamba Suma, amefariki dunia akiwa nchini Burundi alikokwenda kutafuta maisha.
“Alikuwa kipa mzuri lakini hakudumu sana kwenye mpira wa Tanzania kutokana na ubabaishaji, tunawasiliana na wadau mbalimbali wa soka ili kusaidia kurudisha mwili wake Tanzania.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top