0
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imetoa tahadhari ya uwepo wa vipindi vya mvua kubwa inayozidi milimita 50, katika baadhi ya mikoa hapa nchini.

Katika taarifa iliyotolewa na TMA, maeneo yaliyotahadharishwa juu ya uwepo wa vipindi vya mvua kubwa ni  maeneo ya mikoa ya Lindi na Mtwara pamoja na maeneo ya Morogoro kusini.

Mamlaka imeeleza kuwa hali hii inatokana na kuwepo na kuimarika kwa ukanda wa mvua (Inter Tropical Convegence Zone – ITCZ) na mgandamizo mdogo wa hewa ulioko kwenye mkondo wa bahari wa Msumiji.

TMA imezitaka mamlaka husika, wadau wa mazingira pamoja na wakazi wa maeneo husika kuchukua tahadhari stahiki na kuendelea kufuatilia taarifa zinazotolewa, ili kuepuka madhara yanayoweza kujitokeza kutokana na mvua hiyo.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top