"Tunarudia Kusema Maana Msaliti Hana alama. Kama utakuja kutusaliti Salum hutakuwa salama wewe, watoto wako na hata wale mbuzi wako hawatabaki salama. Hatuna muda wa kuchekecheka na wala hatutarudia uchaguzi kwa mambo ya kipuuzi" Bananga.
Bananga amemtahadharisha mgombea huyo kufahamu kwamba kuwa kwake mbunge wa jimbo la kinondoni ni kama vile kufunga ndoa na wana kinondoni hivyo anatakiwa kuwafikisha wananchi hao mahali ambapo walikuwa wanatarajiwa kufikishwa na Mbunge aliyejiuzulu (Mtulia).
Mbali nayo Bananga amemtaka mgombea Mwalimu ahakikishe anakuwa bega kwa bega na wanakinondoni kwenye matatizo na raha zao na pale anapohitajika.
Post a Comment
karibu kwa maoni