0
Image may contain: 2 people, people smiling, outdoor
NAHODHA msaidizi na beki wa kati tegemeo wa Yanga, Kelvin Yon­dani amesema wanataka kuwashangaza mashabiki wao kwa kuweka bonge la rekodi dhidi ya Town­ship Rollers ya Botswana.
Yanga, leo inatarajiwa kujitupa kwenye Uwanja wa Taifa wa Gaborone, Botswana kucheza na Rollers mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Timu hizo zinavaana katika mechi ya marudiano ya raun­di ya kwanza ya michuano hiyo baada ya mchezo uliopita Yanga kufungwa mabao 2-1 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top