0


Mange Kimambi 
Jeshi la polisi Mkoa wa Manyara limewatahadharisha wenye nia ya kutaka kufanya maandamano yanayohamasishwa kupitia mitandao ya kijamii na watu wachache wenye nia mbaya na taifa.
Akizungumza leo wakati  wa mazoezi ya utayari Kamanda wa polisi mkoa wa Manyara Augustino Senga amesema kuwa jeshi hilo lipo tayari kwa kudhibiti vitendo vyote vya uvunjifu wa amani na kwamba yeyote atakaethubutu hatua kali za kisheria zitachukuliwa juu yake.
Kwa mujibu wa taarifa za mitandaoni  ni  Kwamba Mange Kimambi, mwanamitindo aliyebadilika kuwa mwanaharakati wa siasa, ndie muasisi wa maandamano yanayaopangwa nchi nzima kupinga kile anachokiita kuwa ni muendelezo wa ukiukwaji wa haki za binadamu na uminywaji wa haki za kiraia nchini Tanzania.
Maaandamano hayo yamepangwa kufanyika katika siku ya kumbukumbu ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar sherehe ambazo zinatarajiwa kufanyika mkoani Dodoma Kitaifa na kuhutubiwa na Rais John Pombe Magufuli.
Afisa mtendaji wa kata ya Mutuka akitoa maoni yake kuhusu vugu vugu hilo la maandamano amesema kuwa endapo watu watafanya hivyo watatoa mwanya kwa wahalifu kuvunja sheria kiurahisi.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top