0
Image result for magufuli bicha kondoaRais John Pombe Magufuli ameiagiza  wizara ya maji,vyombo vya ulinzi na usalama kuchunguza na kuwachukulia hatua kali za kisheria wote waliohusika na upotevu wa shilingi Bilioni mbili za mradi wa maji wa Ntomboko wilayani Kondoa.
Rais Magufulili amesema kuwa wahusika wa ubadhirifu huo watafutwe popote walipo wakamilishe mradio huo au warudishe fedha hizo.
Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo April 24.2018 Bicha Kondoa alipokuwa akizungumza na wananchi wa Dodoma na Manyara katika halfa ya uzinduzi wa Bara bara ya Dodoma Babati yenye urefu wa Kilomita 251.
Rais Magufuli amesema kuwa wapo watu wasiopenda kuona maendeleo haya yanayofanyika kwa sababu wamezoea kuwaibia wananchi lakini kwa sasa serikali yake haitokubali hali hiyo na kuwataka wananchi wa Manyara na Dodoma kutembea kifua mbele kwa kujivunia Maendeleo.
Walipopata nafasi ya kuzungumza wabunge wa mjimbo manne waliokuwepo kwenye hafla ya uzinduzi wa bara bara,Miongoni mwa wabunge walisimama na kuzungumza ni wa jimbo la Babati mjini [CHADEMA] Pauline Gekul ambapo mbali na kutoa pongezi kwa mradi huo wa bara bara kwa kiwango cha Lami  alimuomba Rais Magufuli kuirudisha stendi ya Babati kwa Halmashauri kutoka CCM  kwani ndio tegemeo la Halmashauri.
Akijibu hilo Rais Magufuli amesema viongozi wa Babati wakae chini na kutatua migogoro iliyopo kwa kuwa nchi ni kubwa sio kila tatizo yeye atatue.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top