0

MTOTO Angela Lucas Abdul (13)[katika picha] anayesoma shule ya msingi Matufa darasa la tano iliyopo kata ya Magugu wilaya ya Babati mkoani Manyara  anaesumbuliwa na tatizo la Macho na ulegevu wa viungo vyake vyote hali inayomfanya ashindwe kuhudhuria shule anaomba msaada kwa wasamalia wema.

 

Akiongea na  mtangazaji wa kipindi cha mtaa kwa mtaa cha Redio Manyara Fm Babati  akiwa ameongozana na bibi yake Hadija Shabani katika ofisi za redio amesema kuwa mjukuu wake alizaliwa akiwa na afya nzuri baadae alianza kupatwa na matatizo hayo.
Bibi anasema kuwa mtoto angela anao wadodo zake wawili ambao nao wanasumbuliwa na matatizo kama hayo.
Kutokana na hali hiyo mama wa watoto hao ambao wote wanasoma inamlazimu kuwapeleka watoto shule asubuhi na kuwapelekea chakula na kuwarudia tena baadae kuwachukua kwani hata kuvuka bara bara au kukimbia hata kujificha wakati wa mvua ni vigumu kwao kutokana na viongo vyao kulegea.
 Bibi yake anasema msaada mkubwa anaoumba ni msamaria mwema ajitokeze na kuwasaidia wajukuu zake wapate shule ya watoto wa aina hiyo yenye bweni na kuwapatia matibabu na mungu atamlipa kwani yeye wala mama na baba yao hawana uwezo.

Aidha bibi wa mtoto huyo anawaomba wasamaria wema kutoa mchango wao wa hali na mali ili afanikiwe kumpeleka Angela kwenye matibabu na kupata shule ya bweni,kiwango cha fedha kinachohitajika hadi sasa hajafahamu.
 Kwa watakao guswa na tatizo la mtoto Angela watoe michango yao kwa simu namba ya VODACOM M PESA  0756294847 ya bibi yake.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top