Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa kampuni
ya uchimbaji ya Acacia, Balozi Juma Mwapachu amestaafu nafasi hiyo
baada ya kuitumikia kwa vipindi viwili.
Mwapachu amechukua uamuzi huo leo,
Julai 13 baada ya muhula wake wa pili wa miaka mitatu mitatu wa ujumbe wa bodi
hiyo, kumalizika.
Taarifa iliyotumwa leo na Bodi ya Wakurugenzi
na Menejimenti ya Acacia imeeleza kuwa inamshukuru Balozi
Mwapachu kwa utendaji wake na ushirikiano wake wote alipokuwa
mjumbe.
“Tunamtakia maisha mema,” imesema taarifa hiyo.
Kutokana na mabadiliko hayo, Bodi ya
Acacia itabaki na wajumbe saba, wakiwamo wanne wakurugenzi na wasio
wakurugenzi.
Post a Comment
karibu kwa maoni