0


Wadau wa Maendeleo mkoa wa Manyara wakisikiliza mada mabalimbali zinazowasilishwa.
Wadau wa Maendeleo mkoa wa Manyara wakisikiliza mada mabalimbali zinazowasilishwa.
July 10 2017, wadau wa Maendeleo wa Halmashauri ya mji wa Babati walikutana na kuajadilim amafanikio na changamoto za utekelezaji wa Mpango na bajeti kwa mwaka 2016/2017 kwa ajili ya Maendeleo y mji wa Babati.
Katika hotuba ya Katibu tawala wa Mkoa wa Manyara Eliakim Maswi iliyosomwa na katibu tawala wilaya ya Babati imeeleza kuwa Halmashauri ilipanga na kutumia Tshs.3,193,04,083/= za mapato ya ndani kwa mwaka wa fedha 2016/2017 ikijumuisha mapato halisi Tshs 2,964,012,797 ysiyo na masharti na Tshs 229,027,286/= mapato yenye masharti.
Taarifa hiyo ilieleza kuwa hadi kufikia mwezi Juni,2017 Halmashauri ilikusanya jumala ya Tshs 1,476,980,365= ya mapato halisi sawa na asilimia 46 ya makisio ya mapato yote ya ndani ikijumuisha Tshs  288,008,578/= za mapato yenye masharti na Tshs 1,188,971,786/= ya mapato yasiyo na masharti.

Tarakimu hizi zinaonyesha kuwa kumekeuwa na changamoto kubwa za makusanyo ya mapato ya ndani kuiwezesha halmashauri kkutimiza malengo yake iliyojiwekea
Nimefahamishwa kuwa kutakuwa na mada itakayowasilishwa  ambayo itaonesha kwa kina maeneo ambayo tumefanya vizuri licha ya changamoto za kibajeti zilizojitokeza.Bajeti hii tuliandaa kwa pamoja hivyo ni vema tukajadili mafanikio na changamoto zilizojitokeza kwa pamoja ili kujua ni jinsi gani tunajipanga kwa mwaka 2017/2018
Ndugu wadau, ni ukweli usiopingika kuwa serikal pekee haiwezi kufanya kila kitu,ndio maana inasisitiza ushiriki wa wadau/sekta binafsi katika shughuli za maendeleo , hivyo mahusiano kati serikali kuu,serikali za mitaa na sekta binafi/wadau lazima yaboreshwe
Napenda kuwafahamisha kuwa maendeleo yoyote duniani hayawezi kuletwa bila kuwepo na amani,nawasihi wote mlioko hapa kwa niaba ya wasiokuwepo humu ukumbuni kuwa mabalozi wazuri wa kuilinda na kuitetea amani yetu kwa nguvu zetu zote Nawaomba mzingatie kwa makini mada zitakazoletwa ili muweze kutoa michango yenu itakayoitoa Halmashauri yetu hapa tulipo nz kuifikisha katika hali bora zaidi
Ni vizuri halmashauri yetu ikachangia kikamilifu katika azma ya serikali ya awamu ya tano ya kuifikisha nhi  yetu kuwa nchi yenye uchumiwa kati ifikapo 2020.
kwa pamoja tulijenge babati yetu.
nawashukuru sana kwa kunisikiliza na kikao chetu nimekifunga rasmi.

ELIACKIMU C. MASWI
KATIBU TAWALA MKOA
WA MANYARA.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top