Uhakika ni kuwa staa wa soka wa England, Wayne Rooney anatarajiwa kutua nchini Tanzania akiwa na kikosi chake cha Everton kwa ajili ya mchezo wa kirafiki dhidi ya Gor Mahia ya Kenya.
Everton inatarajiwa kucheza mchezo huo ikiwa ni maandalizi kujiandaa na msimu ujao wa 2017/18, ambapo timu hizo zinakutana chini ya udhamini wa SportPesa ambao ndiyo wadhamini wa kuu wa Everton.
Rooney mwenyewe amesema safari hiyo itamsaidia kujuana vizuri na wachezaji wenzake.
Post a Comment
karibu kwa maoni