Dkt.
Kijaji ameeleza kuwa nafasi ya wataalamu wa mipango katika kukuza uchumi wa nchi
ni kubwa na kwamba kinachotakiwa ni kuandaa mipango shirikishi itakayochangia
kuimarisha maisha ya wananchi ili waweze kujikwamua kiuchumi.
“Ni
matumaini yangu makubwa kwamba kuzinduliwa kwa kitabu hiki cha mwongozo kwa
wanamipango, kutakuwa chachu ya wataalamu wetu kuangalia namna ya kupeleka
maendeleo vijijini na sehemu nyingine duniani kwa kutoa wataalamu waliobobea
ili kuharakisha maendeleo ya nchi” alisistiza Dkt. Kijaji
Ameeleza kuwa maudhui
ya kitabu hicho yapelekwe hadi ngazi za chini kupitia Serikali za Mitaa ili
watu wengi waweze kukisoma na kuelekezwa namna bora ya kupanga mipango yao ya
maendeleo.
Kwa upande wake Kaimu
Mkuu wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijini, Prof. Hozen Mayaya, amesema
kitabu hicho kimelenga kuwaongezea ujuzi wataalamu wa mipango kwa kuzingatia
vitendo zaidi badala ya nadharia.
“Kitabu cha Mwongozo
kwa wanamipango kitakuwa rejea ya nadharia nyingi na njia ambazo wataalamu wanapaswa
kuzijua, namna ya kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kuifanya mipango iweze
kutekelezeka kama ilivyokusudiwa” alisema Prof. Mayaya.
Nae Kaimu Balozi wa
Uholanzi nchini Tanzania, Bi. Lianne Houben, ambaye kwa namna moja au nyingine nchi
yake imefadhili uandishi na uchapaji wa mwongozo huo, toleo la pili, amesema
nchi yake inajivunia uhusiano imara uliodumu kwa miongo kadhaa na Tanzania.
Alisema kuwa mtazamo
wa ushirikiano wake na Tanzania kuanzia mwaka huu ni kujikita zaidi katika
uhusiano wa kibiashara na kiuchumi na kwamba uwekezaji wao mkubwa utalenga pia
kuboresha kilimo na usalama wa chakula.
“Uholanzi ni nchi ya
pili katika kufanya biashara na Tanzania ikitanguliwa na Marekani ambapo mwaka
2016, Uholanzi, imenunua bidhaa zenye thamani ya Euro bilioni 85” aliongeza Bi.
Houben
Aidha, alieleza kuwa
nchi yake imetoa mchango mkubwa katika kuendeleza rasilimali watu ambapo hadi
sasa wanafunzi na wataalaamu katika fani mbalimbali wapatao 5,000, wamepata
mafunzo kutoka katika vyuo mbalimbali nchini Uholanzi.
Post a Comment
karibu kwa maoni