0
Ameandika Winny ole Sirikwa mkurugenzi wa huduma ya mtoto [COMPASSION] kituo no TZ 204 Monduli kwenye ukurasa wake wa facebook.
Image may contain: 1 person, sitting
Kwanini kila mwanaume anahitaji mwanamke bora? Nimekua katika hii industry ya kuandika masuala ya mahusiano na Ndoa kwa muda kiasi, nimefanya tafiti binafsi mbalimbali za mahusiano.
Nimeongea na watu waliofanikiwa kimaisha na nikajiridhisha na kitu kimoja: Yale maandiko yanayosema "Apataye mke apata kitu chema;
Naye ajipatia kibali kutoka kwa Mungu." Ni ya kweli kabisa.
Mke..nikisema mke namaanisha mke bora huja na kibali cha mafanikio katika maisha ya mwanaume. Nimegundua kwamba kuna level fulani ya mafanikio Mungu hataiachia kwa mwanaume mpaka aoe.
Wanaume wengi wanatamani na kuota mafanikio na Mungu bila shaka huwaangalia na kuwaambia.."Oa na utapata kibali cha mafanikio unayoyataka..."
Mwanamke utakaemuoa anaweza hata asijue mipango yako ya mafanikio. Lakini kwa ule uthubutu wa kumuoa inatosha. Kuna baraka ambazo amezibeba ambazo hazitaachiliwa kwako mpaka awe mke wako.
Anaweza akawa ni girlfriend wako wa muda mrefu, lakini hutagundua thamani aliyonayo mpaka awe mkeo.
Kuna nguvu kubwa sana kwa mwanamke alie bora. Kuna utajiri na mafanikio kwenye ndoa iliyo na mwanamke bora. Ndio maana Mungu mwenyewe founder wa ndoa anasema "Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye."
Mtu huyu mwanaume akiwa peke yake atafirisika..peke yake ni majanga makubwa..peke yake akili yake itavurugwa na slay queens.
Huyo mwanamke wako bora uliyenae anayo nguvu..ila nguvu hiyo itaonekana pale utakapomvalisha pete ya ndoa kidoleni na ukasimamia kiapo chako cha ndoa. Natamani kila mwanamke angefahamu jinsi alivyo full loaded with potentials.
Na ninatamani wanaume wasije wakajilaumu huko mbeleni kwa kuwaacha wanawake bora na kuwaparamia wanawake vipusa, pasua kichwa!

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top