0

Ukosefu wa waalimu maalumu kwa ajili ya kuwafundisha wanafunzi walemavu shuleni imetajwa kuwa ni changamoto kutokana na  mahitaji ya wanafunzi kuwa makubwa kuliko wanafunzi walioko.

Hayo yamebainika katika shule ya msingi Katesh A iliyopo mkoani
manyara wilayani Hanang’ inayofundisha wanafunzi walemavu na wale wasiowalemavu kwa kuwatengea madarasa maalumu pale wanapoanza kusoma kwa mara ya kwanza na baadaye  wakielewa madarasa ya awali ndipo huwachanganya  na wanafunzi wenzao wasio na ulemavu wa aina yeyote.

Shule ya msingi kateshi A ni shule pekee mkoani manyara yenye
kufundisha wanafunzi walemavu wa aina zote  na wengine wakiwa wanakaa shuleni huku wengine wakiwa ni wale wa kwenda na kurudi  naa aina ya walemavu ni walemavu wa akili,walemavu wa macho na viziwi  lakini changamoto zimekuwa ni nyingi kwa wanafunzi hao ikiwemo watoto wengi walemavu kufichwa majumbani na wazazi wao.

Wakizungumza na wanafunzi  hao shuleni hapo umoja wa  wakuu
wakinamama shule za sekondari  wilaya ya Hanang [UWAWASHUKA] walikuwa wakitoa msaada wa vitu mbalimbali vya kula  walieleza kuwa wameguswa na  kile wanachokifanya shuleni hapo na kuonekana kufanikiwa kwa kiwango kikubwa kutokana na kupokea wanafunzi hao bila kujali aina ya ulemavu walionao.

Bi.Esther Malongo ambaye ni mwalimu  mkuu wa sekondari ya  Nagwa  na Mwenyekiti wa chama hicho alieleza kuwa  ni wakati wa wazazi sasa kuwatoa watoto hao kutokuwafungia ndani  na badala yake wawalete waje kuungna na wenzao ili waweze kufuta ujinga  kwani wanahaki ya kupata elimu ambayo ndio mkombozi na mrithi wao kwa ajili ya kesho.

‘’Tumekuja kuwatembelea sisi kama wazazi wenu na kuwahamasisha ili mpate amani na msijione mko tofauti sana na wenzetu hapana  wote mko sawa na  leo tumewaletea zawadi ili ziwasaidie  lakini sisi kama wazazi wenu tunawapenda  na tunataka msome mfike mbali ili muwe mfano wa kuigwa kwa wenzenu ambao hawajaja shuleni lakini pia muwambie wazazi wenu wasiwafungie ndani  wawalete shuleni’’alisema Bi. Malongo.

 Licha ya shule hiyo kuwa na wanafunzi walemavu lakini walemavu hao wanatajwa kuogoza katika  masomo yao  kila mwaka na wameongoza zaidi katika miaka yote toka kuanzishwa kwa madarasa  maalumu kwa ajili ya wanafunzi walemavu mwaka 1996 na waliofeli kwa kipindi chote hicho ni wanafunzi wanne  toka kuanzishwa kwake.

 Naye katibu wa chama hicho cha walimu wakuu wa kike wa sekondari Hanang’ ambaye pia ni mwalimu  mkuu wa  sekondari ya Masqaroda Bi.Gisela  Msoffe  alileza kuwa  shule ni kiwanda kinachozalisha kupitia elimu na ili malighafi yako iweze kuuzika na kupendwa na wengi lazima iwe bora  na huu ndio wakati wa wanafunzi hao  kuweka mkazo kwenye elimu ili waweze kupata  soko.

 ‘’Watoto tunawaomba muache kushaushika  na makundi yaliyopo ambayo yanawapotosha  haswa yale ya utumiaji wa madawa ya kulevya hayo hayfai yatawaharibia maisha yenu kwa haraka  sana  kuweni na  nidhamu ili mzidi kuwa bora zaidi’’Alisema Bi.Esther.

Neema Peter ni mwalimu wa wanafunzi wa walemavu wa akili  shuleni hapo ambaye anaeleza kuwa ukosefu wa walimu  maalumu   ili waweze  kutumia muda kidogo kwenye ufundishaji toofauti na ilivo kwa sasa ambapo hutumia muda mwingi kufundisha kutokana na wanafunzi hao kutumia muda mwingi kwenye kufanya kwa vitendo kuliko kusukiliza.

‘’Hatuzingatii muda maalumu uliotengwa na serikali  kutokana na
uchache wetu walimu  lakini pia hatupo wengi  ni wachache sana hivyo tungeongezewa walimu wengine maalumu  ili tuweze kusaidiana ingetusaidia sana’’alisema Bi. Neema.


Shule ya msingi Katesh A inakabiliwa pia na ukosefu wa vifaa vya
kufundishia  wanafunzi hao hivyo unaiomba serikali kuwasaidia vifaa hivyo pamoja na wadau mbalimbali watakaoguswa kwa ajili ya kuwainua wanafunzi hao ambao  ili waweze kutimiza ndoto zao.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top