Mwigizaji nyota wa Bollywood Sridevi
Kapoor amefariki kutokana na mshutuko wa moyo akiwa na miaka 54, familia yake
imesema.
Mwigizaji filamu huyo ambaye
anafahamika kama Sridevi alikuwa na familia yake mjini Dubai kuhudhuria harusi
wa mpwa wake.
Ameshiriki filamu kwa miongo mitano
katika filamu 300 kama Mr India, Chandni, ChaalBaaz na Sadma.
Alitajwa kuwa mmoja wa wasanii
wachache wa kike waliopata mafanikio makubwa bila ya msaada wa wanaume.
Kutoka akiwa na umri wa miaka minne
alikuwa ameshikiri filamu za lugha za Tamil, Telugu, Malayalam, Kannada na
Hindi
Umati ulikusanyika nje ya nyumba
yake mjini Mumbai wakati habari za kifo chake zilifichuka. Viongozi na wacheza
filamu walielezea kushangazwa na kifo chake.
Waziri mkuu wa India Narendra Modi
aliandika katika mtandao wa twitter kuhusunishwa kwake huku naye rais wa India
Ram Nath Kovind akisema kifo chake kumewavunja moyo mamilioni ya mashabiki.
Post a Comment
karibu kwa maoni