Serikali
imetangaza neema kwa watumishi wake wote wanaoidai malimbikizo ya
madeni kwa kueleza kuwa itaanza kuyalipa madeni hayo ndani ya mwezi huu
wa Februri 2018.
Akizungumza
na waandishi wa habari leo, Waziri wa Fedha na Mipango ameeleza kuwa
mwisho wa mwezi Februari 2018, serikali itawalipa kwa mkupuo mmoja
watumishi wake wote malimbikizo ya madeni na madai yote yaliyoonekana
kuwa sahihi.
“Madai
yanayostahili kulipwa yanajumuisha shilingi Bilioni 16.25 kwa walimu
15,919, na Tsh. Bilioni 27.15 kwa watumishi 11,470 wasiokuwa walimu.
Madai yote yaliyoonekana kuwa sahihi ya TZS Bilioni 43.39 yatalipwa
pamoja na mshahara wa mwezi Februari 2018 kwa mkupuo mmoja,” amesema
Waziri Mpango.
Ameongeza
kuwa kwa malipo ya madai haya ambayo kwa baadhi ya watumishi yana muda
wa zaidi ya miaka kumi, majina ya wadai yatatangazwa kwenye magazeti
kuanzia kesho Jumamosi februari 10, 2018.
“Malipo
ya madai haya ambayo mengine yana zaidi ya miaka 10, majina ya
walipwaji yatatangazwa kwenye magazeti kuanzia kesho tarehe 10 Februari,
2018,” amesema Waziri Mpango.
Waziri
Mpango amesema madai haya yanajumuisha malimbikizo ya mishahara,
nyongeza ya mishahara pamoja na tofauti ya mishahara kutokana na kukaimu
nafasi.
“Madai
haya yalijumuisha mishahara isiyolipwa, tofauti ya mishahara kutokana
na kukaimu na nyongeza za mishahara zilizotokana na kupandishwa vyeo na
kuchelewa kurekebishiwa mishahara… Madai ya watumishi 27,389 kati 82,111
yenye jumla ya shilingi Bilioni 43.39 ikiwa ni 34% ya madai yote,
yalihakikiwa na kuonekana ni sahihi na yanastahili kulipwa bila
marekebisho” amesema.
Aidha
amesema kutokana na zoezi la uhakiki lililofanyika, serikali imeweza
kuokoa kiasi cha shilingi bilioni 84.22 ambazo ni sawa na 66% ya madai
yote zilizokuwa zilipwe kimakosa kutokana na uwepo wa watumishi wengi
wenye vyeti feki.
“Zoezi
la uhakiki wa madai ya malimbikizo ya mishahara uliofanyika, limeweza
kuokoa jumla ya shilingi bilioni 84.22 ambazo ni sawa na 66% ya madai
yote ya malimbikizo ya awali ya shilingi bilioni 127.61 yaliyokuwa
kwenye mfumo… Kama tungekurupuka tu tukalipa, tungekuwa tumetumia vibaya
fedha za watanzania shilingi bilioni 84.22,” amesema Waziri.
Vile
vile amesema kuwa serikali itaendelea kulipa madeni yote ya watumishi
kadiri yanavyojitokeza ili kuepukana na malimbikizo ambayo kwa namna
moja au nyingine, yanaweza kuisababishia serikali hasara.
“Serikali
itaendelea kulipa madai ya watumishi kadiri yanavyojitokeza, ili
kuondokana na malimbikizo ya aina hii ambayo yanaweza kuisababishia
serikali hasara kwa kulipa madai yasiyostahili,” amesema.
Post a Comment
karibu kwa maoni