Dk
Tulia Ackson Mwansasu amempeleka Mbunge wa Iringa Mch Peter Msigwa
kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge ili akatoe ushahidi
wake wa namna ufisadi ulivyofanyika kwenye mradi wa mfumo wa uhamiaji
mtandao (E-Immigration)
Tulia
Ackson amesema hayo baada ya Msigwa kudai kuwa ana taarifa za kutosha
juu ya ufisadi uliofanyika katika mradi uliozinduliwa na Rais Magufuli
hivi karibuni na kudai kuwa Kambi ya Upinzani bungeni wanazo nyaraka za
kutosha ambazo hazina mashaka kuhusu namna ufisadi ulivyofanyika katika
mradi huo chini ya Serikali ambayo inajipambanua kupambana na ufisadi.
Kufuatia kauli hiyo ndipo hapo Naibu Spika aliagiza Mbunge huyo kwenda
kutoa taarifa hizo kwa Kamati ya maadili.
"Mhe.
Msigwa taarifa ulizonazo kuhusu ufisadi uliofanyika kwenye hili zoezi
zipelekwe kwenye hii kamati, Kamati itakuja kulishauri bunge tufanye
nini na huo ufisadi unaoendelea hayo maeneo kwa hiyo naiagiza kamati
imuite Mhe. Peter Msigwa na yeye namuagiza Mhe. Msigwa apeleke huko hizo
nyaraka ili bunge liweze kushauriwa na kuchukua hatua mahususi" alisema
Tulia Ackson.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. John Pombe Magufuli Januari
31, 2018 alizindua Pasipoti Mpya ya Tanzania ya kielektroniki jijini
Dar es Salaam.
Post a Comment
karibu kwa maoni