0
Ni muda mrefu sasa umepita tangu mwanadada wema sepetu akiwa analalamika na kuonyesha kiu yake ya kupata mtoto , baadhi ya watu wamekuwa wakimuonea huruma na wengine kumsema na kumtukana lakini mwanadada huyo hajawahi kuacha kuonyesha kiu yake ya kutaka kupata mtoto.

Akiongea katika chaneli ya EATV,Wema anasema “kwakweli nimekuwa nikitamani kupata mtoto hata leo kwa muda sasa tangu nikiwa na miaka 24 hadi leo nina miaka 29”

Hata hivyo moja ya warembo kutoka kenya aliyekuwa akiishi dubai anaejulikana kwa jina la 2g diva, amejitolea kumsaidia wema kupata mtoto ili kuweza kutimiza ndoto zake za muda mrefu.

Katika moja ya video zilizovuja mtandaon zikimuonyesha dada huyo akiongea anasema kuwa ” wema sepetu darlin suluhisho tunalo, may be unaenda kuwa mama soon”

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top