0
Wabunge wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wametakiwa kutopitisha makubaliano ya kiuchumi kati ya Afrika mashariki jumuiya ulaya [EPA] muswada unaotarajiwa kupelekwa bungeni na kujadiliwa alhamisi ya wiki hii.
Hayo yamesemwa na mratibu wa mviwata Mkoa wa Manyara Martin Pius  wakati akizungumza na manyara fm leo katika mkutano wao mkuu wa tisa wa mtandao wa vikundi vya wakulima Tanzania Mviwata uliofanyika Babati na kuzikutanisha wilaya zote tano za manyara zenye wanachama wa mviwata.
Mratibu huyo ameeleza kuwa endapo wabunge watakubali kupitisha makubaliano hayo ya uchumi Tanzania na jumuiya hiyo ya Ulaya [EPA]yatawabana na kuwaumiza  wakulima kwa kuwa  masharti yake ni magumu.
Hata hivyo mkataba huo unakwenda kujadiliwa huku tayari ikiwa wabunge wameshapatiwa semina kuhusu mkataba huo  wasomi na wataalamu wakitahadharisha Tanzania iangalie faida na hasara kabla ya kuingia kwenye mkataba ambao huenda ukaligharimu Taifa.
Nchi za Afrika mashariki zilizojiunga na EPA ni pamoja na nchi jirani ya Kenya.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top