0
Imeelezwa kuwa ukosefu wa mabweni katika shule za Sekondari zilizopo maeneo ya vijijini ni moja ya vyanzo vinavyochangia Wanafunzi wa kike kushindwa kuendelea na masomo, hali inayopelekea kufifisha ndoto zao.

Hayo yamebainishwa na baadhi ya Wadau wa elimu na wanafunzi wa shule ya sekondari ya GENDA wilayani MBULU mkoani MANYARA wakati wa Harambee ya kuchangia ujenzi wa Bweni la Wasichana wa shule hiyo, ambapo zaidi ya shilingi milioni 45 zimepatikana kutoka kwa wadau mbalimbali.
Mbunge wa Jimbo la HANANG, MARY NAGU amesema njia pekee ya kuondokana na umaskini, jamii inapaswa kubadili mtazamo kwa kuhakikisha mtoto wa kike anapata elimu bora ili kuwa na jamii ya watu wenye uwezo wa kumudu mazingira yao na kuleta maendeleo.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top