0
Image result for RC BENDERAWaziri Mkuu  wa Jamuhuri ya Muungano  wa Tanzania  Mheshimiwa Kassim  Majaliwa (mb) anatarajiwa kufanya ziara ya kikazi ya siku sita Mkoani Manyara  kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya wananchi, kuzungumza na watumishi wa Umma wa Mamlaka ya Serikali za Mitaa na Serikali Kuu waliopo katika Mkoa huo pamoja na kuzungumza na wananchi katika mikutano ya hadhara.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake  Mkuu wa Mkoa wa Manyara Dkt Joel Bendera alisema kuwa  ziara hiyo inatarajiwa kuanza rasmi tarehe 15 februari hadi tarehe 20 mwaka 2017 ambapo pamoja na mambo mengine atashuhudia sala maalumu ya kuombea amani katika  maridhiano ya kuhitimisha uhasama uliokuwepo kati ya wakulima na wafugaji Wilayani Kiteto.
Alisema  Waziri Mkuu akiambatana na Viongozi mbalimbali wa kitaifa  atawasili tarehe 15 februari saa tatu asubuhi Wilayani Kiteto ambapo atalakiwa na viongozi mbalimbali wachama na  Serikali   wakiongozwa na  Mkuu wa Mkoa huo, Katibu Tawala pamoja Kamati za Ulinzi na usalama za  Wilaya na Mkoa .
Pia akiwa Wilayani Kiteto  ataweka jiwe la msingi  mradi wa ujenzi wa ofisi za Halmashauri ya Wilaya hiyo na kuongea na wananchi kwenye mkutano wa hadhara utakaofanyika katika uwanja wa michezo  uliopo mjini kibaya.
Dkt Bendera alifafanua kuwa tarehe 16 februari  Waziri Mkuu atafanya ziara Wilayani Simanjiro  ambapo natapokea taarifa ya Wilaya na kuzungumza na watumishi wa umma katika ukumbi wa Halmashauri hiyo ambapo pia atasalimiana na wananchi wa Mji wa Orkesumrt na kukagua mradi wa upimaji wa viwanja  na kuona mradi wa barabara ya KIA –Mirerani .
Tarehe 17 februari alisema kuwa Waziri Mkuu atakuwa  Wilayani Mbulu ambapo atatembelea Hospitali ya Rufaa ya Haydom  ambapo atapokea taarifa fupi ya hospitali hiyo na kuongea na watumishi wa Umma wa Wilaya ya  mbulu, wananchi wa mji wa mbulu katika uwanja wa Getini.
Tarehe 18 februari Waziri Mkuu atakuwa Wilayani Hanang’ ambapo atapokea taarifa ya Wilaya  na kuzungumza na watumishi wa umma na kuzindua majengo ya madarasa ya shule ya msingi Mogitu na ataongea na wanachi wa Mji wa Kateshi kupitia mkutano wa Hadhara katika uwanja wa shule ya msingi Kateshi.
Aidha akiwa Wilyani Babati tarehe 19 atapokea taarifa ya Wilaya, kuongea na watumishi wa Umma, atakagua mradi wa maji Minjingu, atakagua Kiwanda cha mbolea Minjingu, ataweka jiwe la msingi mradi wa ujenzi wa daraja la Bonga –Endanachani na kuongea na wananchi katika uwanja waq michezo wa Kwaraa.
Tarehe 20 Waziri MKuu atafanya  majumuisho ya siku sita ya ziar4a yake Mkoani Manyara katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa  ambapo Mkuu wa Mkoa huyo aliwataka wakazi wa mkoa huo kujitokeza kwa wingi  kumpokea  kwa kuwa kiongozi wa kitaifa husaidia kushauri na kusukuma  maendeleo  ya Mkoa .

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top