SERIKALI
imetoa onyo kwa watu wanaojihusisha na ujangili na kuwataka kuacha mara moja
kazi hiyo na kutafuta shughuli nyingine, ikisema kamwe hawatakuwa salama.
Akitoa onyo hilo jana
kwenye uzinduzi wa jengo la ukumbi wa kisasa wa maonesho uliopewa jina la Ziwa
Nyasa uliojengwa na Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha (AICC) kwa zaidi ya
Sh bilioni tatu, Profesa Jumanne Maghembe (pichani) alisema mpaka sasa
anawashikilia majangili wakubwa katika magereza mbalimbali nchini.
Alisema
kazi ya ujangili sio salama kwa sasa, kwani serikali inapambana nao usiku na
mchana kuhakikisha inatokomeza majangili wote, kwa usalama wa rasilimali za
Taifa. “Nawashauri
ingekuwa vizuri watu wanaofikiria kufanya ujangili bora watafute kazi nyingine
maana haitakuwa na faida kwao na hawatabaki salama,” alisema.
Aidha alitumia fursa hiyo kuonya wafanyabiashara matapeli katika sekta ya utalii, ambao wanalaghai watalii kwa kuwasiliana nao katika mitandao kuwa wanawaandalia kila kitu na mwisho wa siku wanawaacha kwenye mataa.
Waziri huyo pia amempongeza Rais John Magufuli kwa kukazia mkazo wa kuondoa mifugo hifadhini, kwani ni kweli mtalii akifika hifadhini na kukutana na makundi makubwa ya ng’ombe haileti picha kwake na taswira ya nchi.
Post a Comment
karibu kwa maoni