Wawili hao walionekana na Joop Van Der Linde mgeni katika katika eneo la Ndutu safari Lodge nchini Tanzania katika eneo la uhifadhi la wanyama pori la Ngorongoro.
Simba huyo amepewa jina Nosikitok na ana umri wa miaka mitano.
Simba huyo amewekewa mfumo wa GPS katika shingo yake ili kutambua anakokwenda na ana watoto watatu waliozaliwa kati ya mwezi Juni 27-28.
Daktari Luke
Hunter , ambaye ni rais muhifadhi mkuu wa Panthera ,shirika kuu la ufugaji wa
wanyama aina ya paka aliambia BBC kwamba kisa hicho ni cha kipekee.
Sio kitu ambacho nilijuwa ambapo simba
angeweza kuwalea watoto wa simba mwengine.,...hiki ni kisa tofauti sana.Sina kisa chengine chochote nikijuacho kati ya familia ya mnyama paka kwa mfano pale ambapo mnyama mmoja amechukua mwana wa mnyama mwengine katika familia hiyo hiyo na kumnyonyesha.
Simba wengi wa kike huwauwa watoto wa chui wanapokutana nao, na huwaona kama wapinzani katika mapambano ya kutafuta chakula.
Daktari Hunter anasema Nosikitok ana watoto wachanga walio na umri sawa na mwana huyo wa chui wakiwa na wiki mbili hadi tatu hivi.
Simba huyo alikuwa kilomita moja kutoka kwa nyumba yao ambapo kuna maficho ya watoto wake alipokutana na chuo huyo mdogo.
Alimchukua mwana huyo na kumlea kama wake na humlindi dhidi ya shambulio lolote.
Post a Comment
karibu kwa maoni