BILIONEA
namba moja duniani na Mwanzilishi wa Kampuni ya Microsoft, William Henry
Gates III, ‘Bill Gates’ametua nchini kwa ajili ya kujifunza namna ya
utoaji chanjo kwa magonjwa ya Matende, Mabusha, Minyoo na mengineyo
katika Wilaya ya Muheza mkoani Tanga.
Gates
alifika jana katika Kijiji cha Kicheba na kujifunza namna gani chanjo ya
magonjwa ya Matende, Minyoo, Mabusha na mengine ya aina hiyo
inavyotolewa, kisha akapata chakula na watoto yatima Kata ya Kicheba,
kabla ya saa 7 mchana kurudi tena Tanga mjini.
Hata hivyo,
ujio wake ulikuwa wa kimyakimya bila kuwa na mbwembwe nyingi kama
ambavyo watu wengi wamezoea kuwaona watu maarufu wa aina hiyo wakifanya
ingawa inasemekana anahitaji kuonana na Rais John Magufuli.
Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Hajat, Injinia Mwanasha Tumbo amethibitisha ujio wa bilionea huyo kutembelea wilayani kwake.
“Amekwishaondoka,
ugeni wake ulikuwa ni wa saa chache tu kwa ajili ya kujifunza namna ya
chanjo ya magonjwa mbalimbali inavyotolewa, baada ya hapo akarudi
Tanga."
Post a Comment
karibu kwa maoni