0


Na gharos riwa bunda  0768443315

BUNDA.
Idadi ya wazee wenye umri wa kuanzi miaka 60 na kuendelea wanaoishi katika kata ya Kunzugu Halmashauri ya mji wa Bunda Mkoani Mara, wanaopaswa kupatiwa huduma za afya Bure kwa mujibu wa sera ya serikali bado haieleweki licha ya diwani wa kata hiyo bwana Pasaka Samwel kueleza chanzo chetu cha habari siku kadhaa zilizopita kuwa atalifuatilia   kuhakikisha kuwa wazee  hao wanajulikana kwa majina na kiidadi na waanza kupatiwa huduma hiyo kama kawaida.

Siku kadhaa zilizopita diwani huyo Bwana  Pasaka aliahidi kuwa  atapanga utaratibu wa kukutana na wananchi pamoja na watendaji wake ili kuweka utaratibu wa kuwabaini wazee wenye umri wa kuanzia miaka 60 kwa lengo la kuchukua taarifa zao muhimu na kuziwasilisha ofisi ya mkrugenzi wa halmashauri ya mji huo ili waweze kupata vitambulisho vitakavyowawezesha kupata huduma ya afya bure, lakini hali inaonekana kutoridhisha baada ya taratibu hizo kutozaa matunda na kupatikana taarifa za kumkatisha tamaa diwani huyo.

Akizungumza na chanzo chetu cha habari  kwa njia ya Simu bwana Pasaka amethibitisha  kuwa hajapata jina la mzee hata mmoja kutoka kwa watendaji wake,kitendo kilichomfanya kuwatupia lawama wenyeviti wa vitongoji, wenyeviti wa vijiji pamoja na watendaji kushindwa kuwabaini wazee hao kwakuwa wao ndio wako karibu nao zaidi.

Kuhusu kufanya mkutano katika vijiji vyote vinavyounda kata hiyo diwani huyo amesema tayari walishakutana na kuweka makubaliano kuwa taarifa zifikishwe kwa watendaji ili yeye kama diwani aweze kuzipokea na kuzifikisha halmashauri lakini viongozi hao wameshindwa kufanya kazi hiyo ipasavyo.

Amesema kuwa anashindwa hata afanye nini kuwasaidia hao wazee ikiwa wasaidizi wake ndio wameshindwa kumpa ushirikiano madhubuti wa kuwabaini na kuchukua taarifa za wazee hao.

Hata hivyo amedai kuwa atakachokifanya ni kuendelea kuhimiza suala hili kwa wananchi na viongozi hao ili waweze kuona umuhimu wa kuwasaidia wazee hao ambaoa umri wao umekwenda na hawawezi kufanya chochote zaidi ya kuitaji kusaidiwa zaidi na watu wenye nguvu kama vijana ambao kwa sasa ndio watendaji.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top