Serikali imetoa
shilingi bilioni 5.6 kwa ajili ya kutengeneza bara bara yenye urefu wa km 4.108 mjini Babati kwa
kiwango cha lami katika kipindi cha mwezi novemba mwaka huu hadi novemba
mwakani.
Ujenzi huo
utafanyika kwa awamu mbili ambapo awamu ya pili itakuwa ni zaidi ya nusu.
Fedha hizo
kutoka serikali zimetolewa kwa mkopo wenye masharti nafuu kutoka bank ya dunia
ambapo imetolewa kwa ajili ya kukarabati miji kumi na nane [18] inayoendelea
ikiwemo Babati.
Serikali ya Tanzania imeshiriki asilimia mia moja 100% katika kutekeleza hilo katika miji na majiji.
Akizungumza na
kituo hiki kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya mji wa Babati Bashiri Mhuja amesema tayari wameshafanya makubalianao
na mkandarasi atakaejenga bara bara hizo.
Bara bara
zitakazopitiwa na lami ni pamoja na Maso mapya Nyerere,Mrombo,Mandela na Hango.
Bara bara
hizo zitajengwa kisasa kwa kutengenezwa maeneo ya kuegesha magari [packing]
hivyo kuongeza mapato ya halmashauri ya mji wa Babati na mkoa wa Manyara kwa
ujumla.
Makubaliano hayo ya ujenzi wa Bara bara ya lami katika mitaa ya mji wa Babati pia yameshuhudiwa na mwenyekiti wa Halmashauri ya mji Mohammed Kibiki.
Makubaliano hayo ya ujenzi wa Bara bara ya lami katika mitaa ya mji wa Babati pia yameshuhudiwa na mwenyekiti wa Halmashauri ya mji Mohammed Kibiki.
Kaimu Mkurugenzi
mwanasheria mkuu wa halmashauri,amesema kuwa zipo fursa nyingi zitakazojitokeza
pindi ujenzi unapoendelea na kuwataka vijana na wakina mama,mama ntilie kuzitumia
vizuri fursa hizo kujikwamua kiuchumi.
Mbali na
hayo ametoa angalizo kwa wakazi wa mji wa Babati kujikinga na ugonjwa wa hatari
wa ukimwi kwa kuchukua tahadhari.
Wageni wanapokuja huwa wanakuja na mambo mengine na vishawishi vinakuwepo ila naomba wakazi wa mji wa Babati tuchukue tahadhari.Alisisitiza.
Post a Comment
karibu kwa maoni