0


Image may contain: 2 people, people standingWaziri wa mambo ya ndani Dr.Mwigulu Lameck Nchemba amewataka watumishi wa Mungu na watanzania kwa ujumla kumuombea rais John Pombe Magufuli katika kazi ngumu anayoifanya ya kuitengeneza nchi.
Dr.Nchemba ameyasema hayo jumamosi 25 novemba wakati akizungumza na waumini wa kanisa la KKKT mtaa wa Babati mjini Mkoani Manyara katika ibada maalumu ya changizo la ujenzi wa jengo la kisasa l akanisa katika mtaaa huo.
Naye askofu wa kanisa la KKT  jimbo la kaskazini kati Dr. Solomon Jacob Masangwa amemfananisha rais Magufuli na mhasisi wa kanisa la Lutheran Duniani Martin Luther ambaye alipingwa na watu waovu katika kufanya ujenzi wa kanisa huku akimtaka asivunjike moyo.
Askofu Masangwa ameeleza kuwa kazi anayoifanya rais Magufuli ni kubwa hivyo watanzania wanapaswa kumuombea na kumuunga  ili kukamilisha ujenzi wan chi hii.
Wanaompinga rais Magufuli katika kazi hii kubwa anayoifanya nawafananisha na wale waovu waliokuwa wanampiga vita Martin Luther wakati alipokuwa analijenga kanisa.
Katika harambee hiyo Dr. Nchemba alitoa shilingi milioni kumi katika kuunga mkono ujenzi wa kanisa hilo la kisasa.
Naye mbunge wa viti maalum mkoa wa Manyara Ester Alexender Mahawe akachangia shilingi milioni moja ili kufanikisha ujenzi huo.
Jumla ya fedha zilizopatikana katika harambee hiyo na zilizokuwepo benki ni shilingi milioni 80,
Jengo hilo kubwa la kisasa litakalogharimu zaidi ya shilingi milioni mia tano themanini [580] za kitanzania lenye gorofa moja  lina uwezo  wa kuingiza watu 3,000.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top