0
Image result for DARAJA LA KISASAAhadi ya Rais  mstaafu wa awamu ya nne Jakaya kikwete aliyoitoa  wilayani Mbulu mkoani Manyara, wakati wa kampeni ya kugombea urais mwaka 2005 ya kujenga daraja la mto Magara  ili kuunganisha wilaya hiyo na makao makuu  ya mkoa wa Manyara Babati, imeanza kutekelezwa.

Ni baada ya kukamilika kwa Upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi wa daraja hilo lenye upana wa mita 84 pembeni 24 na katikati mita 36 lililoko umbali wa kilomita 21 kutoka  barabara kuu ya Babati – Arusha, tayari jana Mkandarasi aliyeshinda zabuni ametia saini ya ujenzi wa kivuko hicho.

Akisoma taarifa ya mradi huo mbele ya mwanasheria wa serikali Bi. Emakulata Banzi, wahandisi wa wakala wa barabara TANROADS na wawakilishi wa mkandarasi aliyeshinda zabuni,Meneja wa TANROADS Mhandisi Bashiri alisema Serikali Ilitenga fedha kuanzia mwaka 2007/2008, huku ikiendelea na matengenezo ya maeneo korofi ya mlima Magara.

Alisema Barabara hiyo kupitia daraja hilo ni muhimu kiuchumi kwani imeunganisha hifadhi za taifa za Manyara na Tarangire kwa kupitia Mayoka na kuunganisha mashamba makubwa ya mpunga, mahindi na miwa yaliyopo upande wa pili wa mto kuelekea soko lililoko Babati na Arusha.

Daraja hilo litamalizi kero ya wanafunzi kukosa masomo wakati wa masika, kwani mto huo hujaa maji na husababisha wanaoishi ng’ambo kushindwa kuvuka upande wa pili

Taarifa hiyo iliendelea kwa kusema kuwa zabuni ya ujenzi zilitangazwa tarehe 28 Machi 2017 kwa makandarasi wazalendo na kufunguliwa tarehe 28 Aprili 2017, baada ya uchambuzi wa zabuni aliependekezwa alikuwa M/s Roctronic Limited wa Moshi na hatimaye kujitoa tarehe 02/Juni 2017  kutekeleza mradi huo kwa madai ya kukosa baadhi ya vitendeakazi.

Hatimaye zabuni ilitangazwa kwa mara ya pili ikishirikisha makandarasi wa kimataifa ambapo Mkandarasi M/s China Railway Seventh Group Co. Ltd alipendekezwa kupewa kazi hiyo kwa gharama ya Tsh. Milioni 12,641.244 na mkataba kusainiwa tarehe 14 Desemba 2017 kazi itakayofanywa kwa miezi 24.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top