Uongozi wa klabu ya Lipuli FC umethibitisha kupokea barua kutoka Simba inayomtaka beki Asante Kwasi.
Mwenyekiti
wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe alisema wamepeleka
barua kwa Lipuli FC baada ya kugundua bado ana mkataba na klabu hiyo
pamoja na wakala wake pia.
Lakini leo, Lipuli FC kupitia taarifa katika klabu yao wamesema wamepokea barua na wanaikaribisha Simba mezani.
“Tayari tumepokea barua yao, wanamhitaji Kwasi na sisi hatuna shida, tunawakaribisha mezani.”
Post a Comment
karibu kwa maoni