Na Gharib Mzinga
Binadamu
ameubwa ili aweze kupambana na mazingira yake, Mwenyezi Mungu amempa uwezo wa
kujiongeza
ili aweze
kuishi vema, Kuna baadhi ya watu wakipata changamoto ndogo tu huanza kuonesha
hisia mbaya
Mbele za
watu hata kuchukizwa na kila atendewalo, Katika Soka la Afrika kuna baadhi ya
mataifa
yamekua na
mafanikio makubwa kiasi yanaweza kushiriki michuano mbali mbali ulimwenguni.
(Kichuya
unanielewa?)
Hii
inatokana na uchu wa wachezaji wake walionao, Nchi za Afrika magharibi zimekua
vinara katika kutoa
wachezaji
wengi waliotapakaa Katika ligi zote kubwa ulimwenguni, Huko kote wanatafuta
riziki, kiasi cha
taifa kua na
wigo mpana wa wachezaji, Afrika Magharibi nchi za Nigeria na Ghana huwenda
zikawa mfano
bora kwa
vijana wake kutokata tamaa na kuchangamkia fursa ya Soka popote. (Kichuya
umeelewa?)
Hali hii
tofauti na Nchi za Afrika Mashariki, wachezaji wengi wa nchi hizi wamekua watu
wa kubweteka,
hawajitumi,
Wanalewa sifa huibuka na kuondoka hupotea kabisa, Yupo wapi Said Bahanuzi ?,
Poul Nonga,
Ramadhan
Singano, Abdulrahman Mussa, Abdulhalim Humoud, Hawa ni mfano tu wa wale
waliokuja kwa
mbwembwe
lakini kwa sasa hawajulikaniki walipo. (Kichuya unanipata vizuri?)
Pia wapo
mmoja mmoja ambao wanajitahidi kua na sifa za kiafrika Magharibi, kama vile
Mbwana samata,
Simon msuva,
Thomas Ulimwengu, Abdi Banda na Elias Maguli kwa mbali, Hawa ndio wachezaji
wachache
katika mamia
ya wachezaji wanaopambana na maisha. Mungu awazidishie katika Kutafuta bila
kuchoka.
(Shiza
unawaona hawa?)
Bila shaka
hakuna asiyemjua Victor Moses wa Nigeria na Chelsea, huyu ni mzaliwa wa Nigeria
katika jiji la
Lagos, huyu
alikua winga Machachari kwa vilabu mbali mbali kama vile Crystal palace, Wigan,
westbrom,
Liverpool
Huko kote alikua Winga, Alijituma mno Licha ya kutolewa kwa mkopo Mara kadhaa,
hakukata
tamaa, Ujio
wa Antonio Conte Chelsea umembadilisha kutoka Winga mpaka Mlinzi wa kulia,
Hajawai kuwa
bora kama
alivyokua sasa akicheza nafasi hiyo. Mchezaji tegemezi Katika club.
Mfumo mpya
wa Cattenacio 3-4-3 wa Antonio Conte unamfanya Victor Moses Awe bora na anamsikiliza
mwalimu kwa
kila jambo, kwasasa Anategemewa na kikosi cha Nigeria kuwabeba katika Fainali
za kombe la
Dunia Mwaka
huu. (Shiza unamjua Moses?)
Moses ana
mchezaji mwenzake ambaye wanafanana sana tabia na akili, huyu ni Nicholus Gyan
wa pale
Simba sc (wekundu
wa msimbazi), Huyu alikua Mfungaji Bora huko Ghana katika Club yake ya Dwarf fc
inayoshiriki
ligi kuu Ghana, Simba ikamnunua ili kutatua tatizo lao la Ufungaji, Lakini
amekua hapati
nafasi sana
kama ilivyo kua kwa Victor Moses awali Pale Chelsea, Ujio Wa Masud Djuma na
mfumo ule ule
kama wa
Victor Moses pale Chelsea, Gyan wamekua hatari akiwa kama mlinzi wa kulia.
Amebdilishwa
majukumu kutoka Mshambuliaji mpaka Mlinzi wa kulia, Na ameingia kwenye kikosi
bora cha
mapinduzi
akiwa kama Mlinzi wa kulia. Sababu kubwa ni Tabia za wachezaji wa Magharibi
hufanya jambo
lolote, Gyan
na Victor Moses wamezaliwa Nchi jirani kutoka Lagos mpaka Accra kwa ndege
zinahitajika
kilometa 456
tu, ndio maana wanafanana Tabia.
Kutoka Accra
kwa Gyan mpaka Dar es salaam kilometa 4245, Hapa Gyan anaanzia Wapi kuringa,?
Kutoka
Lagos kwa
Moses mpaka London kilometa 5020 hapa Moses anaanzia wapi kudeka? Hawa
wanatafuta Maisha
Bila
kuchoka. (Shiza, Morogoro Mpaka dar kilometa Ngapi vile?) Utanikumbusha.
Shiza
kichuya ni Miongoni mwa wachezaji Maridadi mwenye uwezo mzuri, Magazeti ya
Bongo yanamwandika
sana kuliko
Magazeti ya London yanavyomwandika Victor Moses. Masikini Gyan Nani
atakuandika? Wewe
wakuja tu
cheza Soka, na usiombe Kuandikwa. Mfumo alioutumia kocha wa Simba sc kule Zanzibar
ndio Ule
unaotumiwa
na Antonio Conte pale Chelsea, 3-4-3 / 3-5-2 Huu hucheza kwa majukumu zaidi
kuliko Namba,
Shiza
kichuya unaonekana Kumchukiza sana, Tangu mchezo wa ndanda Kule mtwara.
Haonekani
kua na furaha, kwakua mfumo Unafanya akae mbali na Goli, Na yeye amehapa kuwa
Mfungaji
bora msimu
huu, Hivyo ndoto zake zinaelekea kukatika, Kutokana na kutofurahishwa kwake
Masud Djuma
ameliona
hilo akaamua kumridhisha kwa kumuweka Namba 9 katika mchezo dhidi ya URA,
Lakini hapo
hakufanya
kitu chochote alikua mtalii tu, Hali iliyopelekea kufanyiwa madiriko.
Baada ya
Mabadiriko Yale Shiza kichuya Alikataa kukaa kwenye Benchi La timu na kwenda
kukaa kwa
mashaki huku
akionekana kuchukizwa na hali hile!!!. Huyo ndio Shiza kichuya mtoto kutoka
Morogoro mji
kasoro
Bahari, na klabu haionekani kama ina mpango wa kumuadhibu maana amefanya
Uvunjifi wa Nidhamu,
Shiza
kichuya hafurahii mfumo wa kocha, Hivyo anaringa, anadeka kujaribu kuonesha
hisia zake kwa
vitendo
mbele ya washabiki pale Amani.
Kipindi
shiza anagomea Benchi, Nicholas Gyan Mshambuliaji wa zamani yupo ndani
anakipiga kisawasawa
kama mlinzi
wa kulia, Amekubali, Na anapambana, Atamringia Nani? Hawezi katolewa akagomea
Benchi
atarudishwa
kwao Mapema sana. (Shiza muangalie mwenzako).
Gyan na
Victor Moses wakupe funzo kwako na kwa Wachezaji wengine wa kitanzania, Chezeni
nafasi yoyote
ambayo
utapewa, hakuna kuchagua nafasi, Kwa namna hiyo kuja kufanikiwa litakua suala
Humu, Victor
Moses
ameshafnikiwa, Gyan amefanikiwa kuwepo kikosi cha kwanza tu, Lakini kwakua
amelipata hilo
ataanza
kutafuta na Mengine.
Huu ndio
utofauti wa wachezaji wa Afrika Mashariki na Afrika Magharibi.
Imeandikwa
Na Gharib mzinga.
gharibmzinga@gmail.com
Post a Comment
karibu kwa maoni