0
 
Mwandishi mkongwe na mpigapicha maarufu zikiwemo zile za michezo, Athumani Hamisi Msengi atazikwa kesho mchana kwenye makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam.

Athumani amefariki dunia leo katika Hospitali ya Muhimbili baada ya kuugua kwa muda wa takribani miaka 10 baada ya kupata ajali ya gari akiwa Kibiti mkoani Lindi.

Taarifa iliyotolewa na familia inaeleza, Hamisi atazikwa kwenye makaburi ya Kisutu baada ya mchusho wa Ijumaa na maandalizi yamekuwa yakiendelea.

Athumani alipata ajali hiyo Agosti 12, 2008 katika eneo hilo wakiwa na waandishi wenzake njiani kwenda Kilwa.
Baada ya hapo alibaki kitandani kwa matibabu Muhimbili, baadaye nchini Afrika Kusini hadi aliporejea nyumbani akiwa na anatumia kiti kutembelea.


Taarifa kutoka kwa ndugu zake zinasema jana mchana alizidiwa ghafla, wakampeleka Muhimbili ambalo alipata matibabu hadi mauti yanamkuta.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top