0

Afisa Mchambuzi Mifumo ya Kompyuta Ndg. Psalm Kisuda pamoja na Afisa Msajili wilaya ya Ikungi mkoani Singida wakiwa katika ofisi ya Usajili mkoa wa Singida wakichapa (printing) taarifa za waombaji Kitambulisho cha Taifa zilizoko kwenye mfumo ili wapate fursa ya Kuzihakiki na kuweka Pingami la Uraia, Umri, Picha, Jinsi na Makazi ya mwombaji sambamba na kuhakiki taarifa za waombaji wengine kama ziko sahihi na kuwafichua wadanganyifu wote endapo watabaini kuwepo kwa waombaji waliodanganya taarifa za uraia wao kwa kujifanya ni raia na kumbe sivyo.

Bi. Catherine Makuri Afisa Msajili  wilaya ya Singida ambaye pia ni mratibu wa shughuli za Usajili Mkoa akibandika taarifa za waombaji shule ya msingi Mangua waliokamilisha maombi ya Kitambulisho cha Taifa wa kata ya Mitunduruni mtaa wa Manguamitogho. Kushoto ni mwananchi akihakiki taarifa zake na Alfa Pius Afisa Msajili Msaidizi akipakaa  gundi kwenye karatasi hizo.

Wananchi wa kata ya Mitunduruni mtaa wa Manguamitogho mkoani Singida wakihakiki taarifa zao za maombi ya Kitambulisho cha Taifa waliyoyafanya ili Kuweka Pingamizi la Uraia, Umri, Picha, Jinsi na Makazi ya mwombaji sambamba na kuhakiki taarifa za waombaji wengine kama ziko sahihi na kuwafichua wadanganyifu wote endapo watabaini kuwepo kwa waombaji waliodanganya taarifa za uraia wao kwa kujifanya ni raia na kumbe sivyo.
Afisa Mchambuzi Mifumo ya Kompyuta Ndg. Psalm Kisuda akitoa Kitambulisho cha Taifa kwa Bi Rabia aliyekamilisha Usajili awali na kukamilisha hatua zote ikiwemo ya Uhakiki na Uwekaji Pingamizi.

Bi. Catherine Makuri Afisa Usajili  wilaya ya Singida ambaye pia ni mratibu wa shughuli za Usajili Mkoa akielekezana jambo na Afisa Uhamiaji Ndg. Hussein Mkuku juu ya kuhakikisha zoezi la Uhakiki na Uwekaji Pingamizi kwa wananchi mkoani Singida linakamilika kwa mafanikio hususan kwa kubaini wale wote waliodanganya taarifa za uraia iwapo watakuwepo.
Katika hali inayoonyesha kasi ambayo Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) inaenda nayo mkoani Singida imeanza kuendesha zoezi hatua ya 3 ya Usajili kwa wananchi kupewa fursa ya Kuhakiki na Kuweka Pingamizi baada ya kukamilisha hatua ya kwanza ya ujazaji fomu na ya pili ya uchukuaji alama za vidole kwa wananchi mkoani humo. 
 
Hatua hiyo  inamhusisha mwananchi kuhakiki taarifa zake juu ya maombi ya Kitambulisho cha Taifa aliyoyafanya awali  zilizobandikwa kwenye vituo vya Usajili katika kata, mitaa na vijiji wanakoishi. 

Taarifa ambazo mwananchi atatakiwa kufika na kuzihakiki ni zinazohusu: Makazi, Uraia,  Umri, Jinsi,  Picha na Jina la Mwombaji  iwapo zinasomeka kwa usahihi.

Bi. Catherine Makuri Afisa Usajili, wilaya ya Singida ambaye pia ni mratibu wa shughuli za Usajili Mkoani Singida amesema katika mkoa wake kwa sasa wameingia katika hatua ya tatu ya Usajili inayojulikana kama Uwekaji Pingamizi ambapo mwananchi anapata fursa ya kuhakiki taarifa zake alizozijaza za Uraia, Umri, Picha, Jinsi na Makazi ya mwombaji sambamba na kuhakiki taarifa za waombaji wengine kama ziko sahihi na kuwafichua wadanganyifu wote endapo atabaini kuwepo kwa waombaji waliodanganya taarifa za uraia wao kwa kujifanya ni raia na kumbe sivyo.


Aidha Bi Makuri Amewataka wananchi wote wa mkoa wa Singida ikiwemo wa Halmashauri ya Manispaa ya Singida katika kata za Mughanga, Mitunduruni, Minga, Utemini, na Ipembe ambazo zoezi hili limeanza kujitokeza kwa wingi kuhakikisha wanahakiki taarifa zao ili Vitambulisho vitakapotolewa viwe vimebeba taarifa sahihi ya waombaji.

Zoezi la Uwekaji Pingamizi katika wilaya ya Ikungi kata za Iyumbu, Ighombwe, Mwaru, Irisya, Mang`onyi, Unyahati, Dungunyi na Ikungi linaendelea vizuri na wananchi wamejitokeza kuhakiki taarifa zao.
 Watendaji wa Vijiji tunaendelea kushirikiana nao kutoa taarifa kwa wananchi ili wafike kwenye vituo vya Usajili ambapo taarifa hizo za waombaji kwa ajili ya Kuweka Pingamizi zimebandikwa. Ameyasema hayo Afisa Msajili Wilaya ya Ikungi Bi Agnes Mtei.

Bi Neema Chaurembo Afisa Msajili wilaya ya Mkalama ameeleza kuwa kwa wilaya yake wamekamilisha Usajili katika Kata sita za Mwanga, Mkalakala, Ilunda, Kikhonda, Kinampundo na Nduguti ambapo maandalizi ya kuwezesha kuanza kwa zoezi la Uwekaji pingamizi katia wilaya yake yako katika hatua ya mwisho hivyo mwanzoni mwa wiki ijayo taarifa za uwekaji pingamizi zitakuwa zimeshabandikwa kwenye kata zote.

Kwa wilaya ya Manyoni zoezi la Usajili Vitambulisho vya Taifa kwa mfumo wa mkupuo limeshakamilika. Katika kata ambazo bado kufikiwa za mkoa wa Singida zikiwemo na zile za wilaya ya Iramba zitafikiwa karibuni hivyo waandae viambatanisho muhimu na vya kutosha vinavyohitajika katika Usajili Vitambulisho vya Taifa. 

Zoezi la Usajili wa Mkupuo linafanyika mkoani Singida  kwa kwa awamu kwa kata ili kutoa fursa kwa wananchi kuweza kuendelea na shughuli za uzalishaji hususan kilimo kwa walio vijijini.
Afisa Usajili mkoa Catberine Makuri wa kwanza kulia na Afisa Habari wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA)Bi Agnes Gerald Wakiwa katika kipindi cha Asubuhi Standard Redio Fm Singida ikiwa ni sehemu ya kutoa elimu kwa umma na kuwahamasisha wananchi wajittokeze Kuhakiki na Kuweka Pingamizi juu ya taarifa zao walizozitoa wakati wa Usajili. Kushoto ni watangazaji Ndg Emmanuel Mlelekwa na Stella Ngenje.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top