0

Mkazi mmoja mkoani Kigoma aliyejulikana kwa jina la Ndimugwanko Mlovezi anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani humo kwa tuhuma za kumpiga mkewe na kumuua.
Akizungumzia tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma Martin Ottieno, amesema tukio hilo limetokea April 20 ambapo mwanaume huyo alimpiga mkewe Bi. Selina Simon hadi kumuua, akimtuhumu kwa nini anamzalia watoto wa kike pekee.
Kamanda Ottieno amesema mtuhumiwa huyo atafikishwa mahakamni hapo kesho April 24 kujibu mashtaka yake yanayomkabili.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top