0

Image result for KABUL PEOPLE DIED 
Watu wapatao 57 wameuawa baada ya mshambuliaji wa kujitoa mhanga kujiripua kwenye kituo cha kuwasajili wapiga kura katika mji mkuu wa Afghanistan, Kabul.
Shambulio hilo limefanyika baada ya siku kadhaa za utulivu katika mji huo. Watu wengine zaidi ya mia moja walijeruhiwa kwenye shambulio hilo.
 Mauaji hayo yanaweza kuchelewesha uchaguzi wa bunge uliopangwa kufanyika terehe 20 mwezi Oktoba.
 Kundi la magaidi wanaojiita dola la Kiislamu (IS) wamedai kuhusika na shambulio hilo na hivyo kuongeza wasi wasi mkubwa juu ya usalama kabla ya kufanyika uchaguzi huo.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top