0

Waendesha bodaboda nao hawajakubali kuwa nyuma kupitwa na zoezi lililosogezwa hadi mtaani kwao karibu na vijiwe vyao vya biashara hivyo wamejitokeza Kusajiliwa ili kupata Kitambulisho cha Taifa kitakachowasaidia kutambulika rasmi katika taasisi za fedha jambo litakolowasaidia kupata mikopo kirahisi na kujikwamua kiuchumi.
Wananchi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro wameitikia wito kwa kujitokeza Kusajiliwa ili wapatiwe Vitambulisho vya Taifa. Akielezea kushangazwa na mwitiko mkubwa wa wananchi, Afisa Usajili wa NIDA wilaya ya Morogoro ambaye pia ni Msimamizi shughuli za Usajili na Utambuzi wa watu mkoa wa Morogoro Ndg. Sererya Wambura ameeleza kufurahishwa sana na mwitiko wa wananchi kutokana na idadi yao kujitokeza kwa wingi tangu siku ya kwanza kwani kwa siku za nyuma idadi ya wananchi waliokuwa wakijitokeza Kusajiliwa siku za kwanza haikuwa kubwa kutokana na wengi kuwa na utamaduni wa kusubiri siku za mwisho ndipo wajitokeze vituoni kwa wingi. ‘Hadi sasa tumeshakamilisha kata 25 kati ya 29 zilizoko kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro. Kata 4 zilizosalia za vijijini zoezi la Usajili linaendeshwa kuanzia wiki hii.

Naye Mtendaji wa Kata ya Lukobe Ndg. Moses Mangwi amewahimiza wananchi wa kata yake ambao bado Kujitokeza Kusajiliwa, wajitokeze kwa wakati ili kuhakikisha wanatumia fursa hiyo muhimu ili kupata haki yao ya msingi ya Kusajiliwa na kupata Kitambulisho cha Taifa kitakachowasaidia kutambulika na kuondokana na adha ya kutotambulika.
Aidha Ndg. Wambura amewapa angalizo watendaji wote wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kutochukua rushwa wala kutoa tozo wanapowahudumi wananchi katika zoezi la Usajili kwani fomu ya maombi ya Kitambulisho cha Taifa na huduma ya Usajili kwa ujumla kwa mwananchi  haina tozo.
Usajili mbali na kufanyika katika Halmashauri ya Manispaa ya mkoa wa Morogoro unaendelea pia katika wilaya nyingine za mkoa huu wa Morogoro; Mvomero, Gairo, Kilosa, Malinyi na Ulanga.
Waendesha bodaboda nao hawajakubali kuwa nyuma kupitwa na zoezi lililosogezwa hadi mtaani kwao karibu na vijiwe vyao vya biashara hivyo wamejitokeza Kusajiliwa ili kupata Kitambulisho cha Taifa kitakachowasaidia kutambulika rasmi katika taasisi za fedha jambo litakolowasaidia kupata mikopo kirahisi na kujikwamua kiuchumi.
 
Bibi aliyezaliwa miaka 41 iliyopita - Shabani Hassan mkazi wa Mtaa wa maduka kumi Halmashauri Manispaa ya Morogoro naye alikuwa mstari wa mbele kuelewa umuhimu wa kutambulika hususan kundi  rika la wazee hivyo kujitokeza Kusajiliwa ili apatiwe Kitambulisho cha Taifa kitakacho msaidia kattika kupata stahiki za wazee kama vile huduma za Afya n.k kirahisi.


Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top