0


Umoja wa wanawake Tanzania [CCM] mkoa wa Manyara umeguswa na watoto yatima wanaosoma shule ya msingi ya serikali Bonga Halmashauri ya mji wa Babati na kuamua kujitolea kuwanunulia sare za shule na Viatu.
Februari 3.2018 Umoja wa wanawake waliwatembelea wanafunzi hao katika shule hiyo ikiwa ni katika kusheherekea miaka 41 ya kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi ambapo waliguswa na watoto hao hali iliyowalazimu kurudi tena baada ya kukubaliana pamoja na wabunge wa viti maalum wa Ccm Ester Mahawe na Martha Umbura kuwa wawasaidie wanafunzi hao.
Kwa mujibu wa Katibu wa Umoja wa wanawake mkoa wa Manyara Hainess Munis ameeleza kuwa Wabunge hao kwa pamoja wamekubaliana kuwasaidia watoto hao kwa kuwapatia sare za shule,  viatu na mahitaji mengine.
Watoto hao ambao wameondokewa na wazazi wao wamefarijika kuona jamii ipo karibu nao na kuonekana wakitabasamu.
Mkuu wa shule ya msingi Bonga January Barnabas anasema kuwa kuna jumla ya watoto 37 ambao ni yatima na uwezo wao darasani unaridhisha.
Aidha mkuu huyo amewapongeza wanawake wa umoja wa wanawake wa Ccm Manyara pamoja na wabunge wa viti maalum kwa msaada walioutoa na kuwataka wengine waige mfano huo wa kuwapa msaa hata pindi wanapohitimu elimu ya msingi waweze kuendelea mbele zaidi.
Katika hatua nyingine Chama cha mapinduzi kupitia jumuiya ya wanawake UWT MANYARA Wamemsaidia mtoto Angelina Lucas mwenye miaka 14 mwanafunzi wa darasa la tano shule ya msingi Katesh anayesumbuliwa na tatizo la Macho na miguu kwa kumkatia bima ya afya na kumfungulia akaunti Benki.
Bibi wa mtoto huyo Hadija Shabani anasema ameahangaika kwa muda mrefu kutafuta pesa za matibabu ila kupitia bima waliopatiwa na Ccm anaamini mjukuu wake atapona.

Post a Comment

karibu kwa maoni

 
Top